Watu wengi wanachanganya maana ya maneno haya kwa
nia ya kutetea imani zao potofu. Baada
ya kulichambua kwa kina swala wokovu (kuokoka), hebu sasa tuone utofauti uliopo
kati ya wokovu na swala la kuongoka. Baadhi ya madhehebu ya kikristo,
hudai kwamba kuongoka ni sawa tu na kuokoka. Kiuhalisia haya ni maneno mawili
tofauti kabisa katika Imani. Tukisema mtu ameongoka hatumaanishi ameokoka, japo
kuna mazingira ambayo yanaweza kuleta maana hiyo. Hebu angalia tafsiri
zifuatazo kutoka kwenye biblia ya Kingereza:
“... declaring
the CONVERSION of the Gentiles: and they caused great joy unto all the brethren (Acts 15:3 KJV) Kiswahili chake kinasema, “wakitangaza habari za kuongoka kwao Mataifa; wakawafurahisha
ndugu sana. Katika mazingira haya neno kuongoka linaweza kuwa na maana sawa na
kuokoka kwa sababu wamataifa walitoka kwenye miungu yao na kugeuka kupitia
Injili ya kweli iliyohubiriwa na Paulo na Barnaba.
But I have
prayed especially for you [Peter], that your [own] faith may not fail; and when
you yourself have turned again,
strengthen and establish your brethren. (Luke 22:32 AMP) Mstari huohuo katika tafsiri nyingine unasomeka, But
I have prayed for thee, that thy faith fail not: and when thou art converted, strengthen thy brethren. (Luke
22:32 KJV) Neno Conversion
limetafsiriwa kama kubadili mfumo au matumizi ya kitu (kikawaida), ila kidini
ni kule kubadili dini au Imani mfano kutoka Uislamu kwenda Ukristo.
Katika mstari huu unaomzungumzia Petro, neno
kuongoka limetafsiriwa kama to have
turned again likimaanisha kujirudi au kurejea upya. Kwenye (KJV) –
limeandikwa - art converted likiturudisha kwenye neno la kwenye Matendo
15:3. Katika Luka 22:32 Yesu anamwambia Petro “lakini nimekuombea wewe
(Petro) ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu
zako.
Kwa hiyo neno
kuongoka linaweza kuwa ni kule kuingia au kuhamia tu kwenye dini fulani, au
kubadili imani (kutoka imani moja kwenda nyingine) bila kuleta maana sawa na
neno kuokoka/kuokolewa (Saved) – linalomaanisha kutolewa kwenye maangamizo au
hali ya uharibifu na kuwekwa kwenye usalama. Au kutolewa kwenye mauti (mshahara
wa dhambi), nguvu za giza, na utumwa wa dhambi; na kuingizwa kwenye ufalme wa
Mungu (maisha mapya ndani ya Kristo Yesu). Au kutengwa na dunia kwa ajili ya ufalme
wa Mungu katika Kristo Yesu.
Kama tulivyoona
kwamba kuokoka ni mpango wa Mungu wa kumtoa mwanadamu kwenye dhambi na mikono
ya shetani (Mautini) na kumweka penye uzima (katika ufalme wake). Kuokoka ni
zaidi ya kuongoka, mtu akiokoka maana yake amemwamini Yesu kuwa Bwana na
mwokozi wa maisha yake ila akiongoka anaweza kuwa amebadili tu msimamo au dini huku
akiwa hajamkiri Yesu.
Kwa kifupi neno
kuongoka ni neno la kidini, bali Kuokoka ni Imani kwa Mungu kupitia Yesu
Kristo. Ndiyo maana Yesu hakututuma kuwahubiri watu habari za dini ili
waongoke, bali habari za Ufalme wake (Injili) ili waamini na kubatizwa –
waokoke. Marko 16:16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Kwa hiyo kuokoka ni zaidi ya
kuongoka. Neno la kingereza linalotumika kwenye neno ataokoka si converted bali ni saved. Whoever believes and
is baptized will be saved - (Mark
16:16 NIV).
Wanafunzi wa Yesu (mitume) walipotumia neno
kuongoka, inawezekana walimaanisha kuokoka kwa sababu watu walikuwa wanatoka
kwenye dini ya kiyahudi au kwenye upagani au kwenye miungu yao na kuingia
kwenye kanisa la Kristo ambapo hapakuwa na madhehebu kama ilivyo sasa. Kimsingi,
kuingia kwenye dini si kuingia kwenye wokovu, japo ukishaingia kwenye wokovu ni
lazima uwe na mahali pa kuabudu pamoja na waamini wenzako. Kuongoka
kunakotokana na Injili ya kweli ya Yesu Kristo ndiko kuokoka.
Kazi iliyomtoa Yesu mbinguni na kuja duniani, hata kupata mateso ni kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. Luka 19:10 inasema "Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea." Kuokoa ni kulipa gharama ya upotevu wa mtu. Yesu alifanyika fidia ya dhambi za wanadamu wote. Tunapotubu na kumwamini Yesu kama Mungu, na Bwana katika maisha Yetu tunaingia katika usalama wa milele. Neno linasema, "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake (Wakolosai 1:13). Wokovu upo ndani yake Kristo.
No comments:
Post a Comment