Tuesday, 9 June 2026

A Strong Marriage vs. A Good Family: Understanding God's Order

In many Christian homes, there is a deep desire to build a good family. Parents work hard to provide for their children, maintain a peaceful home, and raise their sons and daughters in the fear of the Lord. While these are noble goals, there is an important truth that believers must understand: a good family is built upon a strong marriage.

From a Pentecostal perspective, marriage is not merely a social institution; it is a divine covenant established by God and empowered by the Holy Spirit. When the marital relationship is healthy, Spirit-filled, and Christ-centered, the entire family benefits. However, when the marriage is neglected, the family foundation becomes vulnerable, regardless of how much attention is given to other family matters.

God's Design Begins with Marriage

Before there was a family, there was a marriage. In Genesis 2:24, God declared that a man shall leave his father and mother and be joined to his wife, and the two shall become one flesh. This principle reveals God's order.

The first human relationship God established was not between parents and children but between husband and wife. The family emerged from the covenant of marriage. Therefore, the strength of the family is directly connected to the strength of that covenant relationship.

Many couples make the mistake of focusing exclusively on their children while neglecting their marriage. Yet God's design teaches us that when the marriage thrives, the family is more likely to thrive as well.

A Strong Marriage Produces a Good Family

A good family is not created simply by having obedient children or financial stability. It is cultivated through a healthy relationship between husband and wife.

Children learn more from what they observe than from what they are told. When they witness love, forgiveness, prayer, respect, and unity between their parents, they receive a living example of Christian character.

A strong marriage provides:

- Spiritual stability

- Emotional security

- Healthy communication patterns

- A model of godly love

- A peaceful environment for growth

The family becomes a reflection of the relationship that exists between the husband and wife.

The Role of the Holy Spirit in Marriage

As Pentecostal believers, we recognize that successful marriages cannot rely solely on human wisdom. The Holy Spirit must be at the center.

The Holy Spirit helps couples:

- Walk in love during difficult seasons

- Forgive offenses quickly

- Exercise self-control in conflicts

- Pray effectively for one another

- Discern God's direction for the family

A marriage that is continually surrendered to the Holy Spirit becomes a channel through which God's grace flows into the entire household.

Prayer together, worship together, and sensitivity to the leading of the Spirit strengthen the marital bond and create an atmosphere where family members can flourish spiritually.

When Families Come Before Marriage

One of the subtle dangers in modern Christian homes is placing family responsibilities above the marriage relationship itself.

Parents may become so occupied with children, work, ministry, or financial concerns that they neglect nurturing their relationship with one another. Over time, emotional distance develops, communication weakens, and the marriage suffers.

Ironically, efforts to create a good family can unintentionally weaken the very foundation that sustains it.

Wise couples understand that investing in their marriage is not selfish—it is one of the greatest gifts they can give their children.

Christ as the Model of Marriage

Ephesians 5 presents Christ's relationship with the Church as the model for marriage. Husbands are called to love sacrificially, and wives are called to respond with respect and partnership.


A Christ-centered marriage is characterized by:

- Mutual honor

- Sacrificial love

- Humility

- Faithfulness

- Commitment to God's purposes

When these qualities are present, the family experiences the blessing of divine order.

Building Both a Strong Marriage and a Good Family

The question should not ultimately be "strong marriage versus good family." God's desire is for believers to have both.

However, the pathway to a good family begins with a strong marriage. Couples should intentionally:

1. Prioritize their relationship with God.

2. Pray together consistently.

3. Communicate openly and honestly.

4. Resolve conflicts biblically.

5. Spend quality time together.

6. Demonstrate love and respect daily.

7. Allow the Holy Spirit to guide their home.

As the marital covenant grows stronger, the family naturally benefits from that strength.

Conclusively, A good family is a blessing, but a strong marriage is the foundation upon which that blessing rests. God's order has never changed. The health of the home begins with the health of the covenant between husband and wife.

As Pentecostal believers, we must depend on the Holy Spirit to strengthen our marriages, deepen our love, and establish our homes on biblical principles. When marriage is honored and nurtured according to God's design, families become places of peace, discipleship, and spiritual growth. May our homes reflect not only good family values but also strong, Spirit-filled marriages that glorify God and impact future generations.


Saturday, 10 January 2026

SIFA ZA KIONGOZI BORA

 Kiongozi ni mtu aliyejitoa au aliyeminiwa na kupewa dhamana ya kusimamia, kutoa dira na kuonyesha mfano wa jinsi mambo yanapaswa kufanyika. Kuwa kiongozi si jambo rahisi, wala si jambo gumu. Si rahisi kwani linahitaji kujitoa kikamilifu ili maono au malengo yapate kufukiwa, na si gumu kwani si kila kiongozi ni kiongozi. Kukubali nafasi tu hakumfanyi mtu kuwa kiongozi. 

Kukubali nafasi pamoja na kukamilisha majukumu ya nafasi hiyo ndio uongozi. Kiongozi ni lazima awe na uwezo wa kuwashawishi wengine na kuwafanya wawe tayari kutekeleza majukumu yanayolenga kutimiza malengo. Mfano mzuri wa kiongozi ni Musa, yeye alifanikiwa kuwashawishi wana wa Israeli kuondoka Misri na kwenda Kanaani. Mfano mwingine ni Yesu, yeye aliwaongoza wafuasi wake kwa kuonyesha mfano katika mambo yote. Yesu alikuwa kiongozi mwenye ushawishi mkubwa sana. Ushawishi wake ulitokana na uwezo wake wa kufundisha, uwezo wake wa kutatua matatizo ya watu, na ujasiri wa kuwaita wengine katika wajibu aliokuwa nao. 

Mara nyingine aliwaita wanafunzi wake wamfuate, japo wengi walimfuata pasipo hata kuwaita. Baada ya maelezo haya mafupi napenda kukupa sifa kadhaa za kiongozi bora:

1. Kiongozi ni mtu anayejitambua. Yeye ni nani, ana wajibu gani, ana mapungufu gani na ana uwezo (strength) gani. Si mtu anayefanya mambo kiholela. Kila alifanyalo huwa na sababu. 

2. Ni mtu anayeweza kusimamia mambo yake mwenyewe, yakiwemo masomo, familia, biashara, kazi nk. 

3. Ni mtu wenye upendo na watu. Kiongozi asiye na upendo hawezi kujitoa kwa dhati kwa ajili ya watu wake. Yesu alikuwa tayari hata kufa kwa ajili ya watu. Ni mtu anayewatanguliza wengine. 

4. Kiongozi ni mtumwa wa wengine. Mtu asiyetaka kutumikishwa na maswala ya wengine jawezi kuwa kiongozi

5. Mtu mwenye maono au anayejia maono anayotakiwa kuyasimamia. Maono hutoa mwelekeo, na majukumu muhimu yanayohitajika. Kiongozi asiyejua maono hataweza kuwapanga watu wake ipasavyo, wala hawezi kuweka vipaumbele.

6. Mtu mwenye uwezo wa kuwashawishi wengine. Je, maisha ya mtu yanadhihirisha nini? Je, ni mtu anayeweza kuaminika na wengine. Maneno na matendo yake yanaashiria uwezo alionao? Je, ana karama au vipawa gani? Ongea yake inadhihisha hekima kwa kiasi gani? Je, anaweza kuwavutia wengine? Bila ushawishi kiongozi ni mtu aliye na cheo tu. Uongozi mzuri ni ule unaotokana na uwezo wa mtu, kielimu, kiakili, au kiroho. 

7. Uongozi unahitaji kutokuwa mbinafsi na kujua kuwainua wengine. Kiongozi ni lazima awe tayari kuwapa wengine nafasi, na kuwainua. Kiongozi anayejiangalia mwenyewe tu si kiongozi. Tamaa sio sifa ya kiongozi bora. Kiongozi bora hufurahi wengine wakifurahi, na kuhuzunika wengine wakihuzunika. 

8. Kiongozi ni mtu mwenye hekima na busara. Si mtu wa hasira na kukurupuka. Anaweza kutatua shida za watu. Tena ni mtu mwenye utulivu katika kukabiliana na changamoto. Si mtu wa malalamiko. Musa aliweza kusimama katikati ya watu wenye manung'uniko kwa kumtegemea Mungu na kuwahimiza watu wasichoke. Kiongozi mwenye busara hapendi mashindano, magomvi na mivutano.

9. Kiongozi bora ni mfano bora. Kila anachokifanya ni kielelzo cha mafanikio. Ni wa kwanza kwenye kila jambo liwe gumu au jepesi. Si mtu wa maneno tu, bali ni mtu wa vitendo. 

10. Kiongozi ni mzazi na mlezi wa viongozi wengine. Kiongozi asiyezaa na kulea viongozi wengine hana sifa ya kuwa kiongozi. Kuzaa viongozi huthibitisha kuwa yeye ni kiongozi (mtoto wa nyoka ni nyoka). Kuwalea  iongozi huthibisha ushawishi wake kwa wengine. Viongozi hupenda kukaa nyuma ya viongozi.

11. Kiongozi bora ni mcha Mungu. Mtu asiyetambua uwepo wa Mungu, na kuheshimu nafasi ya Mungu kwenye maisha yake na ya wengine hawezi kusimama na watu hata wakafikia maono. Mungu ndiye kila kitu kwa watu wake. Hofu ya Mungu humfanya kiongozi kuwa mtu mwenye utu. Imani kwa Mungu ni nguzo muhimu katika kufikia maono yoyote yenye tija kwa wengine. 

12. Kiongozi bora ni mtu mwenye kutunza kumbukumbu. Anaandika maono, mikakati na mambo yanayojitokeza kwenye kazi. Anawakumbuka watu wake. Na anazikumbuka ahadi zake. Ni mtu mkweli, akisema anamaanisha alichokisema. Na anakumbuka alikotoka, si mtu wa kujisahau na kujiona bora kuliko wengine. Ni mtu wa daftari wakati wote.

14. Ni mtu wa watu, na anapenda kufanya kazi kwenye umoja (timu). Ni mtu anayejua naye ni mmoja wa wachezaji kwenye timu, si mtazamaji. Anajali maumivu ya wengine na anaweza kuvaa viatu vya wengine. Ni mtu anayejali jamii, hata akiwa nje ya jamii. Hana makuu, na anapenda kunyenyekea na kuwasikiliza wengine. Si roboti, wala si sanamu. Ni mtu anayeishi kama mtu.

15. Ni mzalendo kwa nchi au taasisi anayoiongoza. Uzalendo ni upendo wa dhati kwa nchi au taasisi. Ni kujitoa kwa kimaanisha kuibeba nchi au taasisi hata kama maslahi binafsi yataguswa. Mzalendo hafurahii udhali au watu kuonewa. Ni mtu anayeweza akupiga kelele kukemea uovu hata akiwa peke yake. Mzalendo anaweka maslahi ya nchi au taasisi mbele. 

Je, wewe ni kiongozi? Je, wewe ni kiongozi bora? Uongozi una nafasi kubwa ya kupoteza, kubomoa au kuharibu taswira ya kesho. Kila mafanikio huanza na kiongozi mwenye maono. Ni maombi yangu kuwa Mungu akufanye kuwa kiongozi bora. Ni wito wangu kwako leo, kwamba usimame kikamilifu ili kuweka msingi wa mafanikio kwa kizazi cha kesho. Je, watoto wetu wanajifunza nini kutoka kwetu? 

Friday, 18 October 2024

MWANAUME KWENYE NAFASI YA "MUME"

Mume ni mwanaume aliyeoa kwa kuzingatia vigezo na taratibu za kijamii, kishria na za kiroho. Mume si rafiki wa kiume (boyfriend), hawara, wala si mzazi mwenza (kwamba tu umezaa naye). Ili mtu awe mume ni lazima akamilishe taratibu za kijamii, za kisheria na za kiroho katika kuanzisha ndoa.

Ndoa kibiblia, ni muunganiko wa kudumu kati ya mtu mke na mtu mume; na mwanzilishi wa muunganiko huu ni Mungu mwenyewe. Katika Mithali 19:14 tunasoma, “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.” Hivyo, katika kuanzishwa kwa ndoa kibiblia ni lazima Mungu ahusike. Tangu Agano la kale hata sasa, tunaona Mungu akihusika kwa ukaribu sana kwenye ndoa. Ndoa ya kwanza aliifunga mwenyewe kati ya Adam una Eva.

Ibrahimu alipewa Sara kuwa mkewe, Isaka alipewa Rebeka kuwa mkewe, Yakobo alipewa Lea na Raheli kuwa wake zake. Hata kama walijihusisha na wanawake wengine, bado hawa walibaki kuwa na nafasi ya pekee kwao. Kwa hiyo, kuwa mume kwa mke si jambo rahisi na la kawaida, ni jambo lenye kusudi la Mungu ndani yake.

Ukifuatilia ndoa hizi niliziozitaja utagundua kwamba familia zilihusika kwa ukaribu sana katika kuianzisha ndoa. Mfano Rebeka aliulizwa na wazazi wake kama yuko tayari kuambatana na yule aliyetumwa kuja kumchukua. “Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda.” (Mwanzo 24:58) Sheri ana kanuni za jamii zao nazo zilizingatiwa kwa karibu sana.

Maagizo ya Mungu kwa Mume

                                                                                      i.          Kuambatana na Mkewe

Makubaliano kati ya mwanaume na mwanamke katika mahusiano siku zote yamekuwa yakizingatiwa. Tangu zamani iliwalazimu, mwanaume na mwanamke kukubali kuambatana pamoja. Kibiblia, mume ni lazima aambatane na mkewe na kumpokea kama sehemu ya mwili wake (Mwanzo 2:24, Waefeso 5:31, Mathayo 19:5). Tangu uumbaji, mwanamke ni sehemu ya mwili wa mwanaume.

Mungu aliuchukua ubavu mmoja wa Adamu na kumuumba Eva. Naye Eva alipoletwa kwa Adamu, kwa furaha, na kwa kumkubali Adamu lisema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.” Kule kutolewa katika mwanaume ndiko kulikomfanya Eva aitwe mwanamke.

Mwanaume akimwona mkewe katika mtazamo huu ni rahisi kuambatana naye. Kuambatana kunahusu mambo yote katika Maisha: yaani kimwili na kiroho. Mume hana maisha binafsi tena, kila kitu ni shirika. Kwa kukazia Zaidi Paulo anasema, “Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.” (1 Wakorintho 7:4)

Kuambatana kati ya mume na mke, ni kwa lazima. Japo changamoto ni kubwa katika kizazi hiki, inawezekana kuliko vizazi vyote. Ile neno aliloambiwa Eva kusema “tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.” Limekuwa gumu kwa wanawake walio wengi. Hivyo mashindano, chuki, na kutendeana kwa hiyana kumetawala kati ya wanaume na wanawake.

Kuambatana ni jambo pana katika Maisha ya wanandoa.  Mume ni lazima akubali na ajitoe:

Kuambatana na mkewe katika kuhudumiana, huku kunahusisha kujitoa kwa kila mmoja kwa mwenzake. Huduma ya tendo la ndoa ni moja ya huduma za msingi katika ndoa. Paulo anasema, “msinyimane” (1 Wakorintho 7:5). Kuhudumiana kiroho na kimahitaji na mengineyo pia ni sehemu ya kuambatana kwa wanandoa.

Kuambatana na mkewe katika kazi; huku ni kuunganisha mikono pamoja katika kuzalisha. Kazi za nyumbani, za kiuchumi, za kanisa na nyinginezo ni lazima zifanyike katika ushirika wa mume na mke katika ndoa. Mke n msaidizi, mume ni mwongoza njia. Wote wawili ni wasafiri katika chombo kimoja kiitwacho ndoa au familia. Kutiana moyo, kusaidiana, kuwezeshana, na kupeana nafasi katika kazi katika kuambatana hakuepukiki.

Kuambatana na mkewe katika mapato na matumizi; hili ni eneo linalohusu uchumi katika ndoa. Kimsingi uchumi wa ndoa hujengwa na mume na mke, hivyo wote ni lazima wahusike vilivyo katika kupata na kutumia mali zinazozalishwa. Japo jukumu la kuzalisha amepewa Adamu, Eva hawezi kujiweka pembeni kwani naye ni msaidizi. Na Zaidi ni mwili mmoja na Adamu.

Kuambatana na mkewe katika huduma na maisha ya kiroho (kiimani): Imani hubeba hatima ya mwanadamu. Tena huathiri maamuzi ya mtu moja kwa moja. Ikitokea mke na mume hawako pamoja kiimani au kihuduma, kuambatana huwa kugumu. Mume ni lazima akubali kuambatana na mkewe katika mambo ya kiroho ili wawe na hatima njema, vivyo hivyo na mke. Maombi, kusoma neno, utoaji, kutumika, na kumtafuta Mungu kwa pamoja ni msingi wa Maisha ya kiroho katika ndoa.

Kuambatana na mkewe katika malezi ya watoto (kabla na baada ya kuzaliwa): huku kunahusisha kupanga idadi ya watoto, aina ya malezi ya kuwapa watoto, jinsi ya kukidhi mahitaji ya Watoto, na jinsi ya kutunza maadili ya familia.  Mambo haya hayawezi kufanyika kwa ufanisi bila maridhiano na maamuzi ya pamoja. Mume bora ni yule anayeweza kusafiri salama akiwa bega kwa bega na mkewe pamoja na Watoto.

Kuambatana na mkewe katika mipango (iweni na nia moja) na kukuza uchumi wa ndoa na familia: katika ndoa ni lazima kupanga pamoja. Mume atoe mawazo yake, mke naye atoe yak wake. Ndoa iliyogawanyika mara nyingi, huanzia kwenye mipango. Mipango ikishatofautiana, matumizi hayawezi kwenda sawa. Kushirikishana mipango ni njia muhimu katika kudumisha kuambatana. Mume ni lazima amshirikishe mkewe mipango yote aliyonayo.

Mume pia ana jukumu kuambatana na mkewe katika matatizo mfano magonjwa, misiba na mengineyo. Mwanaume anayekimbia matatizo, hana sifa ya kuwa mume. Kuoa ni kukubali kuchukua madhaifu ya mke, na kumshirikisha mke udhaifu wako. Kutafuta suluhu ya matatizo ni moja ya jukumu la msingi la mume katika ndoa.

Mungu ni lazima aambatane na mkewe katika kusaidia ndugu na kuwatunza wazazi. Japo hili linakwenda kwa pande zote mbili, ni lazima mume awe mstari wa mbele kuwasaidia ndugu wa mkewe. Kuambatana kunadai kubebeana mizigo. Katika familia zetu za kiafrika tuna majukumu Fulani ambayo hatwezi kuyaepuka, hivyo kusaidiana ni kwa lazima.

Haya ni baadhi ya maeneo ya msingi, yanaweza kuwepo mengine zaidi. Jambo la msingi hap ani kujua kwamba kuwa ‘mume’ ni kuwa mshirika wa karibu na wa pekee kwa mkeo. Mke ameumbwa kufurahia ushirika na kujaliana katika mahusiano. Hajaumbwa kupambana peke yake, hivyo kuambatana naye ni njia muhimu katika kujenga amani ya ndoa. Mume naye hawezi peke yake, hata  Adamu yalimshinda, hivyo ni lazima mke akubali kuambatana na mumewe.

                                                                                          ii.          Kumpenda Mkewe 

Paulo anasema, “Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. (Waefeso 5:28-29)

Hapa Paulo anasema juu ya kuwapenda wake zetu kama miili yetu, hili ni fumbo zito kwa mume. Waume wote tungeweza jambo hili, ndoa zetu zingekuwa paradiso. Kizazi chetu kinashangaza sana, kwani kesi za waume kuwapiga, kuwaumiza, kuwaacha, wakati mwingine hata kuwaua wake zao zimekuwa nyingi sana. Paulo amatuambia “haiwezekani mtu akauchukia mwili wake. Bali huchukua jukumu la Kuulisha na kuutunza.

Kutokea kwa matukio haya mabaya kunadhihirisha kwamba wanaume wengi hawajawapokea wake zao kama miili yao wenyewe au hawana upendo wa kweli kwa wake zao. Mume aliyempokea mkewe kama mwili wake na kumpenda ni lazima awe na upendo ulio hai. Yaani:

v    Upendo kwa mkewe huambatana na kuhakikisha kwamba anakula na anapata mahitaji yake yote (matunzo). Hata kama ana kazi yake usikubali mkeo akajigharamikia kila kitu, tumia fedha yako kumlisha na kumnunulia mahitaji yake. Kumjali mke kimahitaji ni jukumu la msingi la manaume. Mume ni lazima awe na macho ya kuona mahitaji ya mkewe.

Si lazima mke aombe kila kitu. Vitu vingine ukiona anavihitaji mnunulie naye atajisikia kupendwa kila wakati. Kama mume unayempenda mkeo, hupaswi kuishia kwenye maneno tu, ni lazima upendo wako uambatane na kujali mahitaji. Ukumbuke kabla ya kumwoa mkeo alikuwa anapewa mahitaji na wazazi wake na pengine wanaume wengine, au kujihangaikia mwenyewe. Hakikisha unazipa mapengo yote kwa kufanya Zaidi ya wote.

 

v    Upendo unadai kujitoa: Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake. (Waefeso 5:25). Kujitoa ni kwenda Zaidi ya ile hali ya kawaida ya kutimiza majukumu. Unapofika mahali kama mume ukatafuta muda wa ziada, ukafanya zaidi, ukakubali kuumia kwa sababu ya mkeo basi unakuwa unautimiza upendo.

Linapotokea jambo gumu kwa mkeo, hakikisha unakuwa mstari wa mbele kama mume kutafuta utatuzi. Hata kama litakugharimu kupoteza baadhi ya vitu, Mungu atawajalia neema mtapata vingine baada ya jambo hilo kupita. Kazi zipo tu, ila kujitoa kumsaidia mwenzako wakati wa taabu au hata mazuri yenye gharama ni muhimu.

NiIisikia habari za kijana mmoja (mume) ambaye alimwacha mkewe hospitalini akiwa mahututi kwa sababu ya kuogopa hasara ya kazi aliyokuwa anaifuatilia. Mkewe alipotoka hospitalini, alikuwa na uchungu mwingi sana kwa kuona mumewe amethamini kazi kuliko Maisha yake. Kurekebisha kosa kama hilo, ni gharama kubwa kuliko kuacha faida ikapita.

v Upendo unadai kusamehe na kusahau: Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao. (Wakolosai 3:19) Wanaume wasio na moyo wa kusamehe mara nyingi huwatendea wake zao mabaya. Upendo hauhesabu mabaya (1 Wakorintho 13:4 “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya”

Hivyo, mume mwenye upendo ni lazima ajifunze kumsemehe mkewe. Ni muhimu kukumbuka wamba, wanawake ni watu wa mahusiano zaidi kuliko kazi, hali wanaume ni watu wa kazi zaidi. Kupishana katika mazingira kama haya ni kawaida. Wanawake huwa hawapendi kukosea, hivyo kusamehewa wakikosea ni lenye nafasi kubwa kwenye maisha yao.

v    Upendo unadai heshima: Paulo anafundisha  na kusema, “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe. (1 Petro 3:7). Mume ana jukumu la kuitunza heshima ya mkewe kwa kumvisha vizuri, kumpamba, kumwendeleza, kumpa nafasi na kumsikiliza.

Kwa sababu ya maumbile yao au hali ya maisha au historia wakati mwingine mke anaweza kuonekana kama hana heshima. Kwa mume, mke ni lazima awe malikia katika hali zote. Mume hatakiwi kumvunjia mkewe heshima, kwa kwenda nje ya ndoa, vivyo hivyo mke. Kama mume, ni muni kuyaheshimu mawazo ya mkeo, hisia zake, na nafasi yake kwa ujumla.

v    Upendo unaambatana na kumlinda mkeo: Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. (Malaki 2:14-15) Wanapoinuka watu kumshambulia mkeo usinyamaze, usiwape ndugu (wazazi, wadogo zako, dada zako au marafiki) kumshambulia mkeo. Katika changamoto zote, tunza heshima ya mkeo (chukua aibu yake, na Mungu atakubariki). Zaidi sana usimgeuke na kumtendea mambo ya hiana. Mweke mkeo kwenye mzingira salama, na hakikisha anakuwa salama wakati wote.

Kila mwanamume au mwanamke anapaswa kutunza heshima ya ndoa: Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu. (Waebrania 13:4) Usafi wa ndani na wa nje ni muhimu katika ndoa. Usafi wa tabia ni wa muhimu zaidi sana. Tabia za uzinzi na uasherati zimeharibu mahusiano ya wanadoa wengi, na yameleta aibu isiyofutika.

Mambo ya kufanya kama mume ili mkeo akufurahie

Pamojana maagizo haya makubwa mawili tuliyokwisha kuyaona, kuna mambo kadhaa ya kiutendaji yatakayomfanya mume awe mtu wa kutamanika kwa mkewe kila wakati.

1.               Fanya kazi kwa bidi ili kukidhi mahitaji ya familia, kwa kiwango chako. Mke hujisikia salama akiwa na mume mpambanaji na anayezalisha.

2.               Timiza wajibu wako kwa jamii, mfano kanisani au kazini au pale unapoishi. Mke hujisikia vizuri sana akiona mumewe anaheshimiwa na kusemwa vizuri na watu.

3.               Jifunze kumpongeza mkeo akifanya vizuri, na kumkosoa kwa upendo akifanya vibaya. Hili litampa uhakika wa wewe kuambatana naye, hivyo kuvutiwa na wewe zaidi.

4.               Jifunze kumsikiliza na kuongea na mkeo. Hili ni la muhimu sana, mwanamke hujisikia kama malkia akiona mumewe ametulia akimsikiliza. Mume mwema humsikiliza mkewe kwa uvumilivu na busara. Wanawake wengi hupenda kuongea kuliko kusikiliza. Japo wapo ambao hupenda kusikiliza pia, hivyo msome mkeo na kuhakikisha unakwenda naye alivyo.

5.               Msifie mkeo kwa kumpa majina mazuri, sifia umbile lake na kumtia moyo kila wakati. Mwite mkeo “mpenzi, laazizi, malikia, mke; ikiwezekana weka na kiingereza kidogo kama “honey”, “sweetie” “baby” “sweetheart” na mengine. Haya humpa mke ujasiri na kujikubali zaidi, hivyo kila wakati atatamani uwe naye ili umsifie zaidi.

6.               Mnunulie mkeo zawadi za hap ana pale. Hili litampa kukuamini zaidi, na kuona kumbe unamwaza kila wakati.

7.               Jitahidi kumtosheleza mkeo katika tendo la ndoa. Hapa niongee kwa herufi kubwa “kilichomtoa mkeo kwao pamoja na mengine yote, nit endo la ndoa. Hakikisha kama mume unaongeza ufanisi kila siku. Mkeo atakufurahia sana ukimpa kile anachokihitaji chumbani mwako.

8.               Mwamini mkeo, japo wapo wanawake wasioaminika, tunajua aliyetoka kwa Mungu ni wa kuaminika. Mke akiaminiwa kuna asilimia nyingi za kufanya vizuri kuliko asipoaminiwa. Mpe uhuru, akikuambia jambo likubali bila kuona shaka. Kama una shaka na jambo mwambie wazi ili akupe maelezo. Wanawake ni wasiri lakini wapewa uaminifu, ni lazima walipe uaminifu.

9.               Jenga urafiki wa karibu na mkeo, wakati mwingine muwe na muda wa kucheza, kutaniana kidogo, kukumbushana mambo mbalimbali na mengineyo.

10.            Jifunze kumshukuru mkeo kwa huduma anazokupa mfano tendo la ndoa, chakula, kukufulia, kusafisha ndani, kukutunzia vitu, kulea Watoto na mengineyo.

11.            Pale inapowezekana jiepushe na yale asiyoyapenda, na kuweka muda kwa yale anayoyapenda.

12.            Usimtanie kwenye madhaifu aliyo nayo. Ukifanya hivyo unaweza kumuumiza moyo na kuleta hisia tofauti.

13.            Usimlinganishe mkeo na wanawake wengine, mkubali kama alivyo na mzungumzie yeye zaidi ukiwa naye. Epuka kuwasifia wanawake wengine ukiwa na mkeo.

14.            Ipende familia, ikiwa ni pamoja na kuwahudumia watoto na ndugu. Mke hufurahishwa sana na mume anayeipenda familia. Niliongea na binti mmoja akaniambia moja vitu vinavyomuumiza duniani ni kuona baba yake hajali familia yake. Usilete maumivu kama haya kwenye ndoa yako.

15.            Jiamini na simamia maamuzi yako. Mke huwa hapendi kuona mumewe anatawaliwa na watu wengine. Uthabiti na ujasiri wa kuamua humtia moyo mke.

16.            Uwe mkweli kwa mkeo. Hakuna ukweli ambao mkeo anayekupenda kwa dhati atashindwa kuchukuliana nao. Uongo ni sumu mbaya sana, ukimdanganya kisha akaja kuujua ukweli itakuwa mbaya mara mbili ya kumwambia ukweli.

17.            Usikae mbali na mkeo kwa muda mrefu bila sababu za msingi na makubaliano ya pamoja; ikitokea inakulazimu, hakikisha unakuwa na mawasiliano ya mara kwa mara.

18.            Msaidie mkeo kazi za nyumbani, hasa akiwa amelemewa Na majukumu, amechoka, au anaumwa. Hii itmfanya akuone kama rafiki yake wa karibu sana.

19.            Pale inapowezekana, uwe na mtoko na mkeo; mara kwa mara uwe na faragha naye. Huyo ndiye make wa ujana wako. Kuambatana naye, kutembea pamoja naye, kwenda kanisani pamoja naye, kula pamoja naye, na mengine kama hayo, huongeza sana ladha ya mahusiano.

20.            Usiogope kuwa uchi mbele ya mkeo. Kuoga pamoja ni dsturi nzuri kwa wanandoa. Kuwa huru kwa mkeo Ni ishara ya wazi kwamba unamwamini, na umejitoa kwa ajili yake. Hii inaongeza furaha na mahaba kwenye ndoa.

21.            Dumisha ukaribu na mkeo. Usipende kukaa mbali naye muwapo pamoja. Mkumbatie, mbusu, ongea naye kwa kamnong’oneza. Hili litampa kuona kwamba unamkubali Na hatimaye naye atajibu mapigo.

22.            Heshimu hisia zake - usiwe mtu wa kulazimisha mambo bila sababu. Kama Kuna ulazima kwenye jambo Fulani tumia lugha nzuri kulizungumza, mweleweshe. Usitake kusikilizwa wewe tu. Wakati mwingine mwenzako naye ana namna anatamani mambo yaende. Akikuhitaji pia Ni vizuri ukapatikana.

Saturday, 19 December 2020

MGOGORO WA "CASFETA TAYOMI" NA "CASFETA" NI TISHIO KWA KANISA LA KESHO

Wapendwa Nawasalimu katika Jina la Yesu!

Nianze kwa kuuliza "Je! Kristo amegawanyika?" (1Wakorintho 1:13) Je, Yesu wa CASFETA TAYOMI ni yupi, na wa CASFETA ni yupi? Je, ni Yesu wawili tofauti? Kwa nini mgogoro kati ya makundi haya mawili hauishi? Maswali haya yamenijia baada ya kushuhudia visanga kadhaa kwenye shule za sekondari kwa miaka mingi sasa.  Nakumbuka mkuu mmoja wa shule alisema, “katika shule yangu sitaki kusikia mgogoro wowote wa vikundi vya dini, hasa kwa walokole kwa sababu huwa hawapatani siku zote”

Nimekuwa nikitafakari juu ya hatima ya tofauti kubwa zinazojitokeza katika makundi haya mawili yenye jina moja. Nilichogundua ni kwamba hatima yake si njema, zaidi ni kuendelea kuligawa na kulidhohofisha kanisa. Watoto na vijana wakijengwa katika misingi ya migogoro na kutoelewana hawataweza kusimama pamoja tena, labda ifanyike toba na matengenezo mapema. Kwa kipindi kirefu sasa, kumekuwa na migogoro mingi mashuleni na vyuoni ambayo badala ya kutafutiwa tiba ya kudumu, imekuwa ikifunikwa tu ili maisha yaendelee. Kuna mshangao mkubwa kwa wengi juu ya kutokuelewana kwa walokole. Wengi huuliza: "Kama wana Yesu kweli, mbona hawaelewani." Baadhi ya wakuu wa shule wamekuwa wakikosoa vikali hali ya uhasama iliyopo miongoni mwa CASFETA hizi mbili.

Sijataka kuamini kwamba mithali isema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi” itatimia kwetu. Najua viongozi wengi wa kanisa huwa hawapendi mjadala katika swala hili. Naamini hili haliwazuii watu kuendelea kusema kile wanachokiona juu ya kanisa la Mungu. Ili kanisa la Mungu lijengeke katika utakatifu na umoja ni lazima mambo yote yawe sawasawa. Migogoro miongoni mwa vijana waliookoka mashuleni na vyuoni si ishara nzuri. Ni ishara kwamba kuna nyufa ambazo hazijazibwa. Migogoro ikitawala kati ya ndugu, inakuwa rahisi wao kwa wao kuangamizana. Adui pia anapata nafasi kwa urahisi.

Kuwa na vikundi viwili au hata zaidi ya viwili haina tatizo, inaweza kuwa njia nzuri kabisa ya kupanua wigo wa huduma, lakini vikundi hivi ni lazima viwe huru. Maana yake viwe na katiba isiyoingiliana na vingine, vifanye kazi kwa kuheshimu uwepo wa vikundi vingine, kila kimoja kiwe na misingi isiyoshawishi migogoro na vingine. Ni lazima inapotokea Mungu ameamua kupanua huduma amani izidi kuwepo. Paulo na Barnaba walipopishana, hawakuachana kwa ubaya. Kila mmoja alichukua njia yake kwa amani, na hakuna mahali ambapo mmojawapo alisimama kuusema ubaya wa mwenzake.

Hali sivyo ilivyo kwa CASFETA Tayomi na CASFETA: vimekuwa ni vikundi vya kuvunjiana heshima, kusemana vibaya hata kuitana waasi, kushindania matawi, kunyanganyana wahiriki na hata kuvutana wazi wazi.  Nina hakika jambo hili si jema, ni baya na halimpendezi Mungu. Tunapokuwa na viongozi wa wanafunzi wenye uwezo wa kuwasema wenzao vibaya au hata kuwatendea mabaya, hatujengi kanisa. Ujasiri wa kushuhudia unapungua, uwezo wa kuishawishi dunia unapungua.

Maono ya CASFETA zote mbili ni mazuri, na yana nafasi ya kuleta mapinduzi makubwa kwa kanisa. Changamoto ni kwamba hakuna amani kati yao. Kunapokuwa na Kamba inayovutwa na makundi mawili, kila kundi kuvuta kuelekea upande wake. Mwisho wadhaifu wataangukia upande wa wale wenye nguvu. Kiroho hali haiku hivyo! Tuliookoka wote tunapaswa kukaa upande mmoja ili tuzidi kuivuta dunia ije kwa Yesu. Tunapovutana sisi kwa sisi ni rahisi kuangukia upande wa shetani. Kwa nini tuwaache Watoto wetu wazidi kuvutana? Bilas haka kuna ugumu Fulani katika kuamua. Katika kutafakari nimegundua mambo machache:

Kwa nini mgogoro huu ni mgumu?

1.     WANAOGOMBANA WAMETOKA KWENYE FAMILIA MOJA.

Mgogoro kati ya CASFETA (Tayomi) na CASFETA) hauna tofauti na ule wa ndani ya familia. Watoto wanaweza kugombana lakini mwisho wanakutana kwa baba na mama mmoja. Wazazi na walezi wa vijana waliookoka wote walioko mashuleni na vyuoni ni makanisa yetu ya kipentekoste. Wakitoka shuleni wanakutana kanisani pamoja, na mchungaji wao ni mmoja. Kinachoshangaza ni vita na malumbano yanayoendelea kushamiri kati ya watoto hawa. Ile hali ya kugombana shuleni kwa sababu ya vyama na kurudi kanisani kuabudu pamoja inaonyesha udhaifu katika kanisa.

Baadhi ya watu niliowauliza juu ya jambo hili gumu, wamenipa majibu mepesi. Mmoja aliniambia, “Hili jambo limeshindikana huko tulipotokea sidhani kama linawezekana, wanaolisimamia ndio wanaojua zaidi” Nilipotafakari kauli hii nikagundia kwamba hakuna anayetaka kukubali lawama. Kila mmoja anataka aonekane ni mwema huku ukweli akiujua. Kinacholeta shida ni hali ya kutokuelewana ambayo haijapatiwa ufumbuzi. Ninafikiri kuna haja ya kuwapa vijana na watoto wetu mashuleni na vyuoni ufafanuzi wa kina ili wasije wakajikwaa.

Hatari kubwa zaidi inajitokeza pale ambapo Watoto wanakataliwa wanakwenda kwa wazazi kutaka msaada au uwezesho kwa ajili ya huduma. Nimeshuhudia baadhi ya wachungaji wakiwakataa wanafunzi waziwazi kwa sababu wanatoka CASFETA Fulani tofauti na ile anayoitaka yeye. Jambo hili limaleta majeraha kwa vijana wengi. Nilikutana na binti mmoja aliyekwenda kuomba mchango wa Injili kwenye kanisa alilokuwa anaabudu, akajibiwa vibaya akaumia. Watoto wa familia moja wanapokosa upendo wa walezi, au wakabaguliwa kwa namna yoyote ile huleta maumivu.

2.     SABABU YA KUTOFAUTIANA HAIKO WAZI IPASAVYO

Wengi hawaoni umuhimu wa kuwepo kwa mamkundi haya mawili kwa pamoja. Swali rahisi ambalo huuliza ni “Ni kwa nini msiwe pamoja” Ni kweli si lazima kuwa pamoja ikiwa Mungu hajakusudia hivyo, lakini ni lazima tutofautiane kwa amani. Kuna kanuni moja ya kibiashara ambayo nimejifunza kwa wafanyabiashara katika masoko makubwa. Mara nyingi maduka yanayouza vitu vinavyofanana hujikusanya pamoja. Nia yao ni kuwavitua wateja wengi zaidi ili kila mmoja apate. Huwezi kukuta wakigombana, kila mmoja hujitahidi kufanya ubunifu wake kuimarisha biashara yake.

Kwa CASFETA (Tayomi) na CASFETA hali sivyo ilivyo: mvutano ni mkubwa, hakuna anayetaka kumwona mwenzake. Kwenye tawi la CASFETA, CASFETA (Tayomi) akijitokeza ni shida, na vivyo hivyo kwa CASFETA (Tayomi). Kila mmoja anataka atawale yeye. Nilipata mgogoro mmoja wa tawi lililoanzishwa na CASFETA ila hawakujishughulisha kulihudumia, Tayomi walipokuja wakawahudumia na mwisho wakaligeuza tawi. Baadaye CASFETA walipojua, walikuja kwa hasira na kusababisha mgogoro mkubwa. Mambo hay ani chukizo kwa Mungu.

Fundisho linapokuwa moja inakuwa rahisi kwa washirika kuhama kutoka kundi moja kwenda jingine. Wengi waliokuwa katika moja ya makundi haya wakiwa sekondari (O-Level) waliingia kwenye kundi jingine wakiwa A-Level na hawakuona tofauti yoyote. Vijana wengi hawaoni sababu ya kutofautiana japo wameambiwa mengi. Hali ya kutokuwa na sababu za msingi za kutofautiana imeleta ugumu katika kulitangua fumbo hili. Nafikiri ni vizuri sababu zingeangaliwa kwa undani Zaidi ili kuona kama bado zinaweza kueleweka kwa kizazi hiki na kile kinachokuja. Yapo mambo yanayoweza kueleweka kwenye kizazi Fulani na yasiweze kueleweka kwenye kizazi kingine.

Katika mazingira hay ani lazima matengenezo yafanyike ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza kwa kizazi kisichojua chimbuko la jambo. Alipoinuka Farao asiyemjua Yusufu Wana wa Yakobo waliingia kwenye utumwa. Kama sababu zikiwa ni za mtu binafsi, mtu huyo akishaondoka ni lazima aache mateso. Akiwepo anaweza kujirudi na kusema tofauti, asipokuwepo waliopo ni lazima wasimame kuziba nafasi yake.

3.     NI JAMBO LA KIHISTORIA

Kizazi kilichokuwepo wakati makundi haya yanaanza haikosi wanajua mambo mengi kuhusu makundi haya. Kizazi kinachoibuka na vitakavyokuja vitaathiriwa na umbali wa muda, hivyo tafsiri yao juu ya tofauti zilizopo ni lazima iwe tofauti na ya wale walioshuhudia mambo yote yakitendeka. Nilichogundua katika utafiti wangu ni kwamba mgawanyiko juu ya makundi haya uliimarishwa Zaidi na mpasuko uliokuwepo ndani ya kanisa kwa kipindi hicho. Majeraha ya mgogoro mkubwa wa kanisa yaliendelea kuchokonolewa na uwepo wa makundi haya mawili.

Si jambo rahisi kurekebisha jambo la kihistoria. Inagharimu kizazi cha mashuhuda kukaa na kizazi kinachoibuka ili kuweka mambo sawa. Kizazi cha mashuhuda kikiondoka bila kusuluhisha au kuandika ushuhuda wao katika kile kilichotokea ni rahisi kuleta shida kwa kizazi kinachofuata. Ninafikiri kuna haja ya kizazi cha mashuhuda kulitazama jambo hili kwa kina na kupata muafaka wake. Migogoro ikishazoeleka mara nyingi huwa kawaida lakini kiroho ni chanzo cha anguko.

Kila upande katika migongano inayoendelea, hujihesabia haki kihistoria. Hili haliondoi ukweli kwamba mgogoro wowote husababishwa na mambo kutokwenda sawa. Hivyo ni lazima kuna mahali mambo hayako sawa. Mabaya mangi yaliyomkuta Esau katika Maisha yake yalisababishwa na kule kuuza uzaliwa wake wa kwanza. Kwa hiyo watu wasiojua kwamba Esau alishauza uzaliwa wake wa kwanza, ni rahisi kumlaumu Yakobo. Ni muhimu mambo yaliyotokea yakawekwa sawa. Suluhu ya kudumu ikapatikana.

Kanisa kama mzazi na mlezi wa vijana ni lazima linie mamoja, na kuhakikisha linaondoa tofauti zote zinazoleta changamoto miongoni mwa vijana. Ipo sumu mbaya ya matengano na uhasama inaendelea kutafuta njia ya kuvuka kwenda kwenye kizazi kinachofuata. Ninaamini kwa msaada wa Mung una kwa kuunganisha maombi na jitihada za pamoja hatutaruhusu Watoto wetu wakaingia kwenye magumu tuliyopitia.  Ni wito wangu kwa maaskofu wote, wachungaji wote na kila aliye na nafasi katika kanisa la Mungu lililo hai, kwamba tujitoe kuangalia mstakabali wa kanisa la kesho.

Haitoshi kujaza makanisa leo, na kupata sadaka za kutosha leo, na kufurahia mafanikio leo; yatupasa kuiangalia kesho. Uamsho endelevu ni lazima ujengewe misingi itayorithishwa kizazi hadi kizazi. Wasomi wengi wanajikuta hawana mizizi katika Imani kwa sababu hawakupata watu wa kuwalelea walipokuwa mashuleni. Wengi wamejikuta wakijeruhika kwa sababu ya mambo wanayokutana nayo mashuleni na vyuoni. Kama kanisa tukiamua kuiangalia kesho, migogoro kama hii ya CASFETA haitaachwa tu. Ni lazima iangaliwe kwa ukaribu ili kuwapa Watoto wetu fursa ya kupendana, kutumikiana, na kupendwa na wachungaji wote bila ubaguzi.

Mungu akubariki!

Saturday, 14 November 2020

MAISHA YA UNYENYEKEVU NA TOBA

“Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali” (Zaburi 138:6)

Unyenyekevu ni ile hali ya kukubali kuwa chini hata kama una sababu nzuri za kukaa juu. Ni kukubali kukaa chini ya mamlaka au kanuni au sheria au mfumo Fulani kwa nia ya kujenga. Mtu akikubali kukaa kwenye mamlaka ya Mungu, maana yake ni mnyenyekevu kwa Mungu. Katika hali ya ubinadamu, unyenyekevu umahusishwa sana na umaskini kwani mara nyingi mtu mwenye shida analazimika kujishusha kwa wale wenye navyo ili watoke kwenye shida. Kwenye mazingira ya kazi, wafanyakazi hulazimika kunyenyekea kwa mabosi wao ili waendelee kuwa na kazi; kwenye maswala ya kijeshi pia, wakuu hunyenyekewa na wale walio chini yao.

Unyenyekevu tunaojifunza hapa si huu unaosababishwa na mazingira; hapa tunaangalia unyenyekevu kama tabia ya mwamini inayosababishwa na usafi wa moyo. Hakuna mtu anayeweza kukaa na Mungu bila kuwa na tabia hii. Isaya 57:15 inasema, “Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.”

Mtu mwenye kiburi na kujiinua hawezi kukaa na Mungu au kuwa juu au kufanikiwa. Mithali 29:23 inasema “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwe” Nimeona watu wengi wanyenyekevu wakipata heshima sana. Jifunze kwa watumishi wote waliofanikiwa katika Biblia utagundua kwamba hakuna hata mmoja aliyekuwa na kiburi, wote walikuwa wanyenyekevu Mungu akawainua. Hivyo ni lazima sisi kama waamini tujifunze unyenyekevu. Tuwe wanyenyekevu kwa Mungu na kwa watu wanaotuzunguka. Kimsingi, tuwe na maisha ya unyenyekevu.

Unyenyekevu una mambo mengi unafanya katika maisha yetu kama tulivyoona, yaani:

a.       Unatupa nafasi ya kupewa neema na Mungu. Mithali 3: 34 inasema, “Hakika yake huwadharau wenye dharau, Bali huwapa wanyenyekevu neema”

b.      Unatupa kuwa na uhusiano mzuri na wengine: Watu watakuheshimu, utakuwa na ujasiri kwa watu, Watu watakupenda Mithali 15:33 inatuambia, “Kumcha Bwana ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.” Kumbe hakuna heshima bila unyenyekevu kwanza.

c.       Faida kubwa zaidi ni kutupa kukaa na Mungu

 

Unyenyekevu unatupa kuhudumiana: Mtumishi wa Mungu Petro anatuambia, “…Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.” (1Petro 5:5-7) Unyenyekevu ndio chanzo cha kuinuka au kuinuliwa kwa mtu wa Mungu. Yeyote asiye mnyenyekevu hakika atapingwa na Mungu hata kushushwa chini.

Kunyenyekea chini ya mkono wa Mungu utasababisha Mungu atuinue kwa wakati wake. Neema ya Mungu ipo pamoja na wote wanaonyenyekea. Katika Mathayo 23:12 Yesu anasema, “Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa.” Maisha ya kujinyenyekesha ndiyo maisha ya Mkristo. Yesu mwenyewe kama kielelezo chetu alijinyenyekesha hata mauti ya msalaba ndipo sisi tukainuliwa pamoja naye (Wafilipi 2:6-8) Neno linasema, “ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata” (Waebrania 5:8) Baada ya kunyenyekea alikirimiwa jina lipitalo majina yote (Wafilipi 2:9), tena ametufanyia wokovu wa milele hata akatajwa na Mungu kama kuhani mkuu kwa mfano wa Melikizedeki. (Waebrania 5:9)

Hebu tuuangazie macho mfano huu tunaoupata katika Luka 18:10 – 14: “Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”

Hapa tunaona jinsi ambavyo Farisayo alipata hasara kwa sababu ya kiburi, kujihesabia haki kwa kutimiza taratibu za dini. Yeye alijiona “si kama wengine” ni kweli hakuwa kama wengine lakini haikupasa iwe sababu ya kujihesabia haki. Tunapofanya vizuri au kutimiza majukumu Fulani katika kanisa Mungu anategemea tuendelee kunyenyekea na kuwathamini wengine. Mtoza ushuru yeye alijishusha, akakaa mbali kwa unyenyekevu (alipiga magoti) na kumwomba Mungu akimwambia “uniwie radhi mimi ni mwenye dhambi” Hii ndiyo siri ya kufanikiwa kwake. Mimi na wewe leo tunakwendaje mbele za Mungu? Tunawaonaje wengine ambao hawafanyi kwa viwango kama sisi?

Katika kitabu cha 1Samwel 2:3 tunakutana na maneno haya, “Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa maarifa, Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.” Kumbe Mungu ndiye hupima matendo yetu, hatuna haja ya kujisifia kwayo. Tukiyabeba matendo yetu kama sababu ya kujihesabia haki tutajikuta tumebaki wenyewe, kwani hakuna hata tendo moja linalotosha kulipa gharama ya uhai wetu. Ni vema tukamwishia Mungu kwa unyenyekevu, na shukrani kwa yale aliyotuwezesha kufanya.

Mungu hawezi kumwacha mnyenyekevu: “Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.” (Ayubu 22: 29). Hata kama unapita katika magumu kiasi gani, ukiendelea kunyenyekea mbele za Mungu kwa moyo uliopondeka hakika Mungu hatakuacha. Daudi alipoona ameanguka, hakuanza kujitetea. Alishuka akamlilia Mungu kwa kuyararua mavazi yake (ishara ya unyenyekevu), na Mungu akamsamehe. Kutenda dhambi kisha ukaficha na kujifanya mtakatifu si Ukristo huo, ni unafiki mbaya, ni kiburi. Ni vema ukajinyenyekesha ukaomba Mungu akusamehe, utakuwa salama.

Angalia mafanikio yasiufanye moyo wako ukainuka ukamsahau Mungu aliyekutoa kwenye utupu na kukubariki (Kumb. 8:11-14). Watu wengi huwa wanyenyekevu wakiwa hawana kitu ila wakifanikiwa wanapoteza heshima kwa Mungu na watumishi wake. Maisha yetu kama waamini hayapaswi kuwa hivi. Tunapaswa kuendelea kunyenyekea hata kama tutabarikiwa kwa kiasi gani. Mungu anataka tutafute pamoja naye, tumiliki pamoja naye, tutumie pamoja naye na tuendelee kuishi pamoja naye hata tukipoteza. Maisha ya Ayubu yanatufundisha somo la unyenyekevu mbele za Mungu.

Maisha baada ya kuokoka ni maisha ya unyenyekevu kwa Mungu, kwa viongozi wa kanisa, kwa watu wanaotuzunguka kulingana na Neno la Mungu. Ndani ya maisha ya wokovu tunapaswa kuwa na mioyo ya toba na unyenyekevu. Kila wakati tuhitaji rehema za Mungu, na kumtii Mungu kutoka moyoni. Tuwape heshima viongozi na kuwasikiliza katika mapenzi ya Mungu. Petro anaagiza na kusema, “ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

Unyenyekevu unatupa kuweza kuhudumiana: Katika kanisa sisi ni viungo, kila mmoja na mwenzake; hivyo hatuwezi kuepuka kuhudumiana. Katika unyenyekevu kila mmoja wetu akiwatanguliza wengine, tutahudumiana. Paulo anaeleza jinsi ambavyo amekuwa  “akimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote” (Matendo 20:19) Je, sisi tunatumika kwa jinsi gani? Nabii Sefania anasema, “Utafuteni unyenyekevu” (Sefania 2:3) Huwezi kuwa mhudumu ndani ya nyumba ya Mungu, na ukatumika kwa mafanikio, bila kuwa mnyenyekevu. Jifunze unyenyekevu. Paulo anahitimisha kwa kusema, “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.” Wafilipi 2:3

 

KUOKOKA NI ZAIDI YA KUONGOKA

Watu wengi wanachanganya maana ya maneno haya kwa nia ya kutetea imani zao potofu.  Baada ya kulichambua kwa kina swala wokovu (kuokoka), hebu sasa tuone utofauti uliopo kati ya wokovu na swala la kuongoka. Baadhi ya madhehebu ya kikristo, hudai kwamba kuongoka ni sawa tu na kuokoka. Kiuhalisia haya ni maneno mawili tofauti kabisa katika Imani. Tukisema mtu ameongoka hatumaanishi ameokoka, japo kuna mazingira ambayo yanaweza kuleta maana hiyo. Hebu angalia tafsiri zifuatazo kutoka kwenye biblia ya Kingereza:

... declaring the CONVERSION of the Gentiles: and they caused great joy unto all the brethren (Acts 15:3 KJV) Kiswahili chake kinasema, wakitangaza habari za kuongoka kwao Mataifa; wakawafurahisha ndugu sana. Katika mazingira haya neno kuongoka linaweza kuwa na maana sawa na kuokoka kwa sababu wamataifa walitoka kwenye miungu yao na kugeuka kupitia Injili ya kweli iliyohubiriwa na Paulo na Barnaba.

But I have prayed especially for you [Peter], that your [own] faith may not fail; and when you yourself have turned again, strengthen and establish your brethren. (Luke 22:32 AMP) Mstari huohuo katika tafsiri nyingine unasomeka, But I have prayed for thee, that thy faith fail not: and when thou art converted, strengthen thy brethren. (Luke 22:32 KJV) Neno Conversion limetafsiriwa kama kubadili mfumo au matumizi ya kitu (kikawaida), ila kidini ni kule kubadili dini au Imani mfano kutoka Uislamu kwenda Ukristo.

 Katika mstari huu unaomzungumzia Petro, neno kuongoka limetafsiriwa kama to have turned again likimaanisha kujirudi au kurejea upya. Kwenye (KJV) – limeandikwa - art converted likiturudisha kwenye neno la kwenye Matendo 15:3. Katika Luka 22:32 Yesu anamwambia Petro “lakini nimekuombea wewe (Petro) ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

Kwa hiyo neno kuongoka linaweza kuwa ni kule kuingia au kuhamia tu kwenye dini fulani, au kubadili imani (kutoka imani moja kwenda nyingine) bila kuleta maana sawa na neno kuokoka/kuokolewa (Saved) – linalomaanisha kutolewa kwenye maangamizo au hali ya uharibifu na kuwekwa kwenye usalama. Au kutolewa kwenye mauti (mshahara wa dhambi), nguvu za giza, na utumwa wa dhambi; na kuingizwa kwenye ufalme wa Mungu (maisha mapya ndani ya Kristo Yesu). Au kutengwa na dunia kwa ajili ya ufalme wa Mungu katika Kristo Yesu.

Kama tulivyoona kwamba kuokoka ni mpango wa Mungu wa kumtoa mwanadamu kwenye dhambi na mikono ya shetani (Mautini) na kumweka penye uzima (katika ufalme wake). Kuokoka ni zaidi ya kuongoka, mtu akiokoka maana yake amemwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake ila akiongoka anaweza kuwa amebadili tu msimamo au dini huku akiwa hajamkiri Yesu.

Kwa kifupi neno kuongoka ni neno la kidini, bali Kuokoka ni Imani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo. Ndiyo maana Yesu hakututuma kuwahubiri watu habari za dini ili waongoke, bali habari za Ufalme wake (Injili) ili waamini na kubatizwa – waokoke. Marko 16:16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Kwa hiyo kuokoka ni zaidi ya kuongoka. Neno la kingereza linalotumika kwenye neno ataokoka si converted bali ni saved. Whoever believes and is baptized will be saved -  (Mark 16:16 NIV).

Wanafunzi wa Yesu (mitume) walipotumia neno kuongoka, inawezekana walimaanisha kuokoka kwa sababu watu walikuwa wanatoka kwenye dini ya kiyahudi au kwenye upagani au kwenye miungu yao na kuingia kwenye kanisa la Kristo ambapo hapakuwa na madhehebu kama ilivyo sasa. Kimsingi, kuingia kwenye dini si kuingia kwenye wokovu, japo ukishaingia kwenye wokovu ni lazima uwe na mahali pa kuabudu pamoja na waamini wenzako. Kuongoka kunakotokana na Injili ya kweli ya Yesu Kristo ndiko kuokoka.

Kazi iliyomtoa Yesu mbinguni na kuja duniani, hata kupata mateso ni kutafuta na kuokoa kile kilichopotea. Luka 19:10 inasema "Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea." Kuokoa ni kulipa gharama ya upotevu wa mtu. Yesu alifanyika fidia ya dhambi za wanadamu wote. Tunapotubu na kumwamini Yesu kama Mungu, na Bwana katika maisha Yetu tunaingia katika usalama wa milele. Neno linasema, "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake (Wakolosai 1:13). Wokovu upo ndani yake Kristo.

A Strong Marriage vs. A Good Family: Understanding God's Order

In many Christian homes, there is a deep desire to build a good family. Parents work hard to provide for their children, maintain a peaceful...

Powered By Blogger