Tuesday, 21 July 2015

Masomo/shule na wokovu

 Kikawaida kila mazingira huwa na changamoto za aina yake kwa mtu aliyeokoka, aliyeko kwenye biashara ana za aina yake, aliajiriwa naye vivyo hivyo, iwe ni mjini au kijijini, shuleni au nyumbani. Vilevile mfumo unaoweza kumfanikisha mtu unatofautiana kulingana na mazingira na changamoto; na kila changamoto zina jinsi ya kukabiliana nazo.
Ninaposema masomo namaanisha masomo ya kawaida ya darasani ambayo huwa tunayaita hasa shule. 
Unapokuwa masomoni ni lazima ujue kwamba kusimama katika wokovu kuko palepale, hautaweza kujitetea kwa lolote mbele za Mungu endapo utauacha wokovu. Haijalishi masomo yanaonekana magumu kiasi gani, bado Mungu anatarajia kupata matunda mazuri kutoka kwako katika hatua hiyo ya maisha. 
Katika kipindi hiki tulichonacho cha mapinduzi makubwa ya kisayansi na teknolojia pamoja na kampeni kubwa ya utandawazi (Globalization); vijana wengi walioko masomoni wamepoteza mwelekeo wa maisha yao ya kiroho.

MWANAUME KWENYE NAFASI YA "MUME"

Mume ni mwanaume aliyeoa kwa kuzingatia vigezo na taratibu za kijamii, kishria na za kiroho. Mume si rafiki wa kiume (boyfriend), hawara, wa...

Powered By Blogger