Si jambo rahisi kupata tafsiri ya maisha, japo wengi hufikiri kwamba wanajua sana maisha hasa kwa sababu ya kuwa na Umri mkubwa au kuwa na vitu fulani ambavyo wengine hawana. Je, maisha ni nini? Vijana wengi huondoka vijijini na kwenda mijini wakisema wanakwenda "kutafuta maisha..............." Je maisha hutafutwa?
Maswali haya ndiyo natamani yatujengee mwelekeo mmoja wa kuyaendea maandiko ili tuone ni nini Mungu anasema kuhusu maisha.
Kumb. 4:9 "Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako"
Zab 9:11 Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa; Na miaka ya maisha yako itaongezwa
Luka 12:23 Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
Luka 21:34 Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
Mdo 15:26 watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Mdo 20:24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.
1 kor 6:4 Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa?
1 kor 15:19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.
Filip 1:20 "..................ikiwa kwa maisha yangu, au ikiwa kwa mauti yangu."
1 Pet 4:3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
Saturday, 7 September 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MWANAUME KWENYE NAFASI YA "MUME"
Mume ni mwanaume aliyeoa kwa kuzingatia vigezo na taratibu za kijamii, kishria na za kiroho. Mume si rafiki wa kiume (boyfriend), hawara, wa...
-
“Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali” (Zaburi 138:6) Unyenyekevu ni ile hali ya kukubali ku...
-
Watu wengi wanachanganya maana ya maneno haya kwa nia ya kutetea imani zao potofu. Baada ya kulichambua kwa kina swala wokovu (kuokoka), h...
-
NDOA INAHITAJI USAFI WA ROHO NA MWILI Uchafu ni kitu cha kuchukiza sana. Hakuna mtu yeyote anayeweza kuchukuliana na mazingira machaf...
No comments:
Post a Comment