Wednesday, 21 September 2016

DHAMBI(SIN) NI NINI?


Neno Dhambi linadhihirika katika maandiko kama mjumuiko wa uovu, mabaya, hatia, makosa, ukengeufu na uasi. Vifungu vifuatavyo katika biblia vinatupa upana wa tafsiri hii:
Zaburi 51:1-9
“Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa (Transigressionon)yangu. Unioshe kabisa na uovu (iniquity) wangu, Unitakase dhambi (Sin) zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu.
Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani. Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; Nawe utanijulisha hekima kwa siri, Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.  Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi. Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; Uzifute hatia zangu zote.”
Maneno ya asili (Ya Kiebrania)yaliyotumika kwenye maneno haya ni
Þ    Kwa neno Makosa (transigression) ni neno ‘peša’ likimaanisha ‘rebelliousness’ kufanya kinyume na utaratibu au uasi.
Þ  Kwa neno Uovu (Iniquity) limetumika neno ‘hātā’ linalomaanisha ‘moral misshapennes’ yaani kinyume na maadili ya ki-Mungu kwa makusudi. Neno hili limetumika mara 580 katika Agano la kale.
Þ    Neno sin limetokana na neno ‘āwōn’ linalomaanisha ‘shorticomings’Kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
Katika Agano jipya yametumika maneno  ya Kiyunani mawili:
Neno ‘adikia’ linalomaanisha kufanya makosa (wrongdoing), kinyume na haki (Unrighteousness), na kinyume na sheria (Injustice). Katika kundi hili, dhambi inaonekana kuwa kitendo cha hiari anachokifanya mtu, kinachoweza kuleta madhara au uharibifu kwa mtu mwingine.
Neno jingine ni ‘hamartia’ ambalo limetafsiriwa mara nyingi kama Dhambi (Sin). Kundi hili la dhambi linajumuisha maneno yote ya Kiebrania yaliyotumika katika Agano la kale (yaani ‘āwōn’, ‘hātā’ na ‘peša’).

Dhambi (Sin) katika agano Jipya inamaanisha kukosa maadili ya ki-Mungu (Makosa), maovu na uasi mbele za Mungu.

1 Yoh. 3:4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi (rebellion). Kuasi ni kukiuka kwa makusudi taratibu au sheria zilizowekwa na mamlaka Fulani, ni kwenda kinyume na maagano au mapatano. Hili tunaliona kwenye kitabu cha mwanzo pale ambapo Adamu na Eva waliamua, japo kwa kudanganywa na shetani, kula tunda la mti ambao Mungu aliwakataza. (Mwanzo 3)
1 Yoh. 5:17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti.
Warumi 14:23 “… Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi.”

Mithali 24:9 Fikira za mpumbavu ni dhambi, Na mwenye mzaha huwachukiza watu.
Mithali 21:4 Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari, Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
Ayubu 23:11 Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.
Kumb.11:28 na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.
Dhambi imetafsiriwa tena kama “Matendo ya mwili”
Wagalatia 5:19 inasema, “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Tena, Dhambi ni Ibada ya sanamu. Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.”

Kuna tofauti kati ya dhambi kwenye Agano la kale na dhambi wakati huu wa Agano la Jipya.
Dhambi katika Agano la kale ilikuwa ni kule kuvunja sheria (Torati ya Musa), na kwenda kinyume na taratibu za dini ya Kiyahudi. Amri kumi za Mungu ndizo zilikuwa kielelezo cha Amri zote. Katika Warumi 4:15 mtume Paulo anatuambia “Kwa sababu sheria ndiyo ifanyayo hasira; maana pasipokuwapo sheria, hapana kosa.” Kwa hiyo kumbe watu walianza kuhesabiwa makosa pale sheria ilipowekwa.

Katika Agano la kale sheria na hukumu zake zilikuwa mikononi mwa waalimu wa Dini na Mafarisayo. Na walikuwa na uwezo wa kumhuku mtu yeyote kulingana na sheria hizo. Kwenye Waebrania 10:28 tunasoma “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.” Kwa hiyo watu wengi walikufa – utaratibu ulikuwa jino kwa jino, atakayeua kwa upanga atauwawa kwa upanga.

Warumi 8:3 Maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili
Wakolosai 2:23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.

Paulo akizizungumzia taratibu za ibada ya Kiyahudi katika Wakolosai 2:23 akasema, “Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
 Katika agano jipya dhambi ina upana zaidi.

Yale yaliyokuwa magumu kwa sababu ya sheria sasa katika Kristo Mungu anayafanya mepesi. Warumi 8:3 inasema “Maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili”

Yesu alitangaza mfumo mpya wa maisha ya Kiroho.
Mathayo 5:23-48 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako……….   Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake……..Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.

Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu. Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino; Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili. Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia. Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili. Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo. Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

Maeneo yaliyopigiwa mstari yanaonyesha hali ilivyokuwa kipindi cha sheria, lakini tunaona Yesu akitangaza mambo mapya na kusema, “lakini mimi ninasema” Kwa hiyo sasa tunasimama katika yale aliyoyasema Yesu yaani; Kuacha na kukaa mbali kabisa na zinaa, kutokuachana, kutokuapa, kuwapenda maadui na kuwaombea.
Tena katika Mathayo 22:37-39 Yesu akatangaza amri kuu mbili, “Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.”

Katika sheria ni hapakuwa na kumpenda jirani kama nafsi, wa kukaa naye ni Yule tu ambaye alikuwa amekubalika kutokana na Torati. Kwa sababu hiyo Wayahudi walilazimika kujitenga na wanadamu wengine wote waliokuwa wanaabudu sanamu. Hapakuwa na kuchangamana.
Yesu alipokuja sasa tunaambiwa:
Waefeso 2:14 Kwa maana yeye (Yesu) ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga.
2 Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Wagalatia 2:16 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

Warumi 6: 17-23 “Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki.  ….  Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa. Kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki. Ni faida gani basi mliyopata siku zile kwa mambo hayo mnayoyatahayarikia sasa?
Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni mauti. Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele. Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”


Thursday, 8 September 2016

FIKIRI TOFAUTI

KWA NINI NIKO HAPA HAPA? 
(Why Am I  here?)

       Hili ni swali ambalo kila mwenye akili atajiuliza akiona amekaa eneo moja kwa muda mrefu bila kuona mabadiliko chanya yaliyokusudiwa au yaliyotazamiwa. Kuna kipindi wana wa Israeli walifika mahali wakawa wanazunguka milima ya Seiri, tena kwa miaka mingi Mungu aliwatokea na kuwasaidia kwa kuwapa mwelekeo mpya. "Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini." (Kumbukumbu 2:3)





      Angalia maneno haya aliyoyasema mwanamashahiri mahiri William Shakespeare ‘There is nothing good or bad, but thinking makes it so.’ kwa kiswahili anasema, "Chochote kiwe kibaya au kizuri, ni mawazo au fikra hukifanya hivyo. Hakika vile unavyofikiri ndivyo utakavyojijenga. Kwani maamuzi ya mtu huongozwa na mawazo ya mtu. Mawazo duni husababisha maamuzi duni. Matendo ya mtu ya leo ni matokeo ya mawazo yake ya jana.





     Biblia inazunguimza juu ya vitu ambavyo humtia mtu unajisi. "Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi." (Marko 7:23), Kwa hiyo kumbe mtu hawezi kuwa mzinzi kama mawazo ya uzinzi hayako ndani yake; tena hawezi kuwa muuaji, mwizi, mkorofi, mlafi nk nk kama hajawahi kuyawaza hayo.





     Hebu nikuulize wewe unawaza nini? Unaweza ukawa unapambana na mambo fulani au tabia fulani ndani ya maisha yako bila mafanikio. Anzia kwenye kubadili jinsi unavyofikiri. Leo nakushauri kama unataka kufanya tofauti, fikiri tofauti. Fikra zako zikiwa zinawaza mambo madhaifu, ugumu, mabaya, maovu na mengine kama hayo bila shaka huweza kuyaepuka mambo haya. Mawazo ya kujidharau yakikutawala hautakaa uheshimike, hashima ya kweli, mafanikio ya kweli huanzia ndani ya mtu. Ili uwaze tofauti kuna mambo ni lazima uyape kisogo, uyaepuke kwa nguvu zote.

Epuka:
1. Kuangalia mambo yaliyopita (your past) na kuvunjika moyo. Huwezi kurudi nyuma kurekebisha makosa ila unweza kujifunza kitu cha kuzalisha (constructive) kutoka kwenye makosa au kufeli huko kulikopita. "Past is past because it has passed, future is future because it is yet to come. Nothing can be changed about past but future is your decision." 
    Kuangalia mambo yaliyopita sio kwamba ni vibaya kwani ni muhimu kuishi maisha ya kujitathmini, tatizo lipo kwenye kuwekeza moyo wako (fikra) zako huko. Waswahili husema, "Yaliyopita si ndwele tugange yajayo" tena wakasema"Maji yakishamwagika hayazoleki" Paulo naye akasema "Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele. (Wafilipi 3:13)

2. Kuwaza mambo manyonge. Mambo makubwa ndiyo yatakayokupa kupanuka kifikra, kiubunifu na hatimaye kiutendaji na Mafanikio. Waza mambo makubwa yanayowezekana, mwamini Mungu na kutenda kwa bidii utafanikiwa.

3. Kuwa na mawazo ya kushindwa. Mawazo ya kushindwa ni sumu ya mafanikio, hata kama umejaribu ukakwama. Jaribu tena na tena hadi uone mafanikio. Mawazo ya kushindwa yatakufanya utangetage hata kukosa kabisa mwelekeo.

4. Kuwaza  maovu na mambo machafu. Mawazo machafu ni kitovu cha maamuzi mabovu. Tunza fikra zako kwa kutazama, kusoma na kusikiliza vitu vya kujenga ufahamu badala ya vitu vya kipuuzi. Soma vitabu, sikiliza wasomi na watu wenye hekima, tazama mambo mazuri achana na marafiki wabaya.

5. Kuchukulia mambo kikawaida. Kumbuka kuna leo na kesho, fanya mambo kwa umakini na maarifa. Ongeza bidii na juhudi zaidi kila siku.
6. Kufanya mambo vilevile kila siku kila wakati. Tafuta kuboresha jambo lako kila siku, litazame ujiridhishe.





Kumbuka Mungu alipomaliza kuumba ulimwengu na vitu vyote, alitazama na akaona kuwa ni vyema. Na wewe jifunze kuyatazama mambo kwa jicho la tathmini.





NENO LANGU KWAKO MPENDWA: 

"FIKIRI TOFAUTI ILI UWE WA TOFAUTI".
Ili ufikiri tofauti:
1.  Yakumbuke makuu ya Mungu ( Yale uliyofanikiwa) na utiwe moyo kwa hayo.
Daudi alipokuta wana wa Israeli na jeshi lote wamenywea kwa jeshi la wafilisti alifikiri tofauti na hatimaye akafanya tofauti. Alitazama mambo makuu ambayo Mungu alimtendea akatiwa nguvu akasimama kumwangusha Goliati. Unapowekeza muda wako mwing kufikiria juu ya mambo uliyoshindwa ndivyo unavyozidi kujidhoofisha.

Wekeza muda wako kuyakumbuka makuu ya Jehova, utasikia kuinuliwa sana. Kazi kubwa ya waliyoshindwa ni kutengeneza hadithi nzuri juu ya kushindwa kwao, bali waliofanikiwa hutengeneza hadithi mbaya kuonyesha sabababu zilizoshindwa kuwafanya washindwe. Majaribu kwao ni mtaji si mateso.

2. Kataa maovu kama Yusufu aliyofanya.
Uovu na dhambi vimezimisha ndoto za wengi. Wengi wameishia mahali duni na pa kukosa tumaini kwa sababu ya kuendekeza maovu. Hakuna raha wala amani kwa watenda mabaya. Mafanikio ya kweli huambatana na wenye haki, wanaowatanguliza wengine. Yusufu alimkimbia mke wa Potifa akaendelea kushikilia maono yake. Majaribu kama hayo ni mengi nyakati hizi lakini ukiamua kukimbia hakika Mungu atakupeleka kwenye ndoto zako. Uovu na nguvu ya kutawala moyo (nia, hisia, na mawazo).

3. Jifunze kutazama fursa mbalimbali na kuchukua hatua.
Usione fursa zote ni za wengine, kaa mkao kutafuta na kuchangamkia fursa. Daudi alipomwona Goliati alitafuta namna ya kuitumia ile fursa kwa kuulizia wengine. Alipochukua hatua ngumu alipanda thamani ndani ya dakika chache. Na wewe usilale, fanya kitu. Pigana na Goliati wetu nasi tutakupa heshima. Hupaswi kulazimisha kuheshmiwa kama wengi wanavyong'ang'ania heshima za vyeo, fanya kitu heshima yako itapanda yenyewe.

4. Ambatana na watu waliofanikiwa zaidi yako kifikra na kimaendeleo.
Watu waliopiga hatua wakati mwingine huwa sababu ya sisi kuvutwa na kufuata nyao zao. Wengi pia hupenda kuwainua wengine. Watu waliofanikiwa wanaweza kukujenga sana kifikra, kwani wengi huwa hawaamini katika kushindwa. Na huwa na mbinu nyingi na shuhuda zenye kujenga sana. Pia, huwa wanakutana na fursa nyingi sana.

5. Fuatilia mambo yenye kujenga (achana na mambo ya kipuuzi)
Tumia muda wako katika mambo ya kujenga, pata taarifa zenye tija. Mawazo ya wengi yamejaa mambo yasiyo na faida kwa sababu ya kusikiliza, kutazama na kusoma upuuzi. Tafuta kanda, vitabu, magazeti na sikiliza vipindi vya maana. Kuangalia ponografi, kusikiliza manyimbo ya kihuni, kushabikia mipira, kubeti, na mengine kama haya ni kupoteza muda wa thamani wa maisha yako.

6. Soma vitabu na kujifunza kila siku.
Kusoma si lazima uende shule, nunua vitabu vya kiroho, vya uchumi, vya kisiasa na vinginevyo ujiendeleze. Mawazo yako yanaweza kunolewa na watu waliofanikiwa kupitia yale waliyoandika. Usiwe mvivu wa kusoma.

8. Mtegemee Mungu na kusoma neno lake kwa bidii.
Mungu ndiye chanzo cha mafanikio yake. na kumcha yeye ni chanzo cha maarifa yote (Mith 7:7). Mtegemee Mungu, usiamgalie mazingira na kukata tamaa, Ishi ahadi za Mungu na uache kufikiri kinyonge. Mungu akiwa upande wetu hatupaswi kuogopa. 

9. Sikiliza mahubiri na kanda za mambo ya kiroho.
Kusikiliza kuna nguvu kubwa sana. unaposikiliza unajipa fursa ya kufikiri na watu waliofanikiwa kupata fikra njema kutoka kwa Mungu. mahubiri yana siri kubwa sana. Pata muda usikilize na Mungu atakupa kufikiri kwa utofauti.

10. Badilisha marafiki ulionao (Achana na marafiki wasiojitambua)
Katika kitabu cha Mithali tunasoma "Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake." Mithali 27:17 Marafiki wa umbea, mizaha, masengenyo, wavivu, wenye wivu, walevi, wazinzi, wezi, wahuni ni kaburi wazi la ndoto zako. Hakikisha kama wewe ni chuma (Strong) unatafuta marafiki chuma ili mnoane. Marafiki wabaya huharibu tabia ya mtu mwema. Watakupotezea heshima. Huwezi kuaminika ukiwa na marafiki wasioaminika. 

Uwe na marafiki wenye fikra za mafanikio, mawazo ya kujenga, wanaojiamini na wanaoamini katika kufanikiwa, wenye imani katika Mungu. Nawe utafikiri kama wao au zaidi yao na kisha utafanikiwa kama wao au zaidi yao.




Katika haya na mengine utakayojaliwa na Mungu kibinafsi, utaanza kuwaza kwa tofauti na baadaye utaamini kwa tofauti, kisha kufanya kwa tofauti na kufanikiwa kwa tofauti.


Mungu akubariki kwa kuwa sehemu ya blog hii. Karibu kwa masomo mengine.

Mwl. Stephen M. Swai
0713511544

THE TRUTH ABOUT SALVATION

Some people in this world weather due to lack of clear knowledge or any other reason, get confused on the term Salvation. Some say it is not possible for a person to be saved. Some think that to be converted to a certain religion or denomination is the same as Salvation. Now, what is it real?

Wow! I’m sure this is right time for God to talk to you about SALVATION in Jesus Christ. Apostle Paul in 2 Corinthians 6:2 says, “I tell you now is the time of God’s favor, now is the day of salvation.” It might be you have heard about Salvation in one way or the other but today is so special for you to hear this Good news about Jesus Christ. 
Salvation is all about Jesus Christ, that is what made Him to come on earth "TO SAVE THE WORLD" in Matthew 1:21, the Angel of God speaks to Joseph about Mary. The Angel says, "She will have a son, and you will name him Jesus-because He will SAVE his people from their sins" 
Then in John 3:16-18 we read "For God so loved the world, that he gave his only begotten Son, that whosoever believeth in him should not perish, but have everlasting life. For God sent not his Son into the world to condemn the world; but that the world through him might be saved. He that believeth on him is not condemned: but he that believeth not is condemned already, because he hath not believed in the name of the only begotten Son of God."

Here you can the Love of God to us human being, because of our sins Jesus is given as a ransom. In 2Peter 3:9 we read, "
The Lord is not slack concerning his promise, as some men count slackness; but is longsuffering to us-ward, not willing that any should perish, but that all should come to repentance"
Remember we are all sinners!
In Romans 3:23 we read that "We are all sinners and we have fallen short of glory of God" Then under sin:
- We were all died (Ephesian 2:1)
- We were darkness (Ephesian 5:8)
- We were under powers of darkness (Colossians 1:13)

In Ephesian 2:8 we read that:

It is grace of God
It is by faith in Jesus Christ we are all saved
In the book of John 1:12 we read, "But as many as received him, to them gave he power to become the sons of God, even to them that believe on his name"
  • In Jesus, we are new creatures: In 2Corithians 5:17 we read "Any one who is joined to Christ is a new being; the old is gone, the new has come"
  • In Christ we have eternal life: Romans 6:23 we read "For the wages of sin is death; but the gift of God is eternal life through Jesus Christ our Lord"
  • We have moved from dearth to life: John 5:24  says "I am telling you the truth: those who hear my words and believe in him who sent me have eternal life. They will not be judged, but have already passed from death to life"
  • In Jesus we are free from slavery of sin. (John 8:31,34-36)

So, salvation is neither church membership nor religion, but the plan of God to save the lost man from bondage of sin. You may be a faithful member of a certain denomination, religion or church but that doesn't guarantee your salvation. 
Salvation is much about restored relationship between sinful man and Holy God through blood of Jesus shaded at the cross of Calvary.  Jesus came for reconciliation between us and Almighty God 
Now is the time for you to make decision, and accept Jesus as your Lord and Savior. 

MWANAUME KWENYE NAFASI YA "MUME"

Mume ni mwanaume aliyeoa kwa kuzingatia vigezo na taratibu za kijamii, kishria na za kiroho. Mume si rafiki wa kiume (boyfriend), hawara, wa...

Powered By Blogger