TAFUTA KUTIMIZA KUSUDI LA MUNGU
KATIKA KILA UNALOLIFANYA.
Utangulizi:
Kila jambo litakalokujia wewe
kama mtumishi wa Mungu jua kwamba lina muunganiko na kusudi unalolitumikia kwa
wakati huo au unaloelekea kulitumikia. Jambo lolote liwe baya au jema, liwe
gumu au jepesi, uwe unalijua au haulijui, liwe la kawaida au lisiwe la kawaida.
Nafasi au fursa zote anazofungua
au alizofungua Mungu kwako , vita anavyoleta shetani, hali ya mwili wako
binafsi-usumbufu, umbo, sura nk; hali ya kiuchumi, familia uliyotoka, maeneo
uliyopita na yote uliyofanya katika maisha uliyoishi ni lazima yawe na matokeo
ya namna moja au nyingine katika kusudi unalotumikia au utakalotumikia.
🔃🔃
Kila mahali Mungu anapokupeleka
ni lazima pawe na kusudi lake, wakati mwingie kusudi lake ni kukuandaa kwaajili
ya kusudi jingine. Kila unalofanya likikufanya utimize kusudi la Mungu rahisi kuona mafanikio makubwa yakiandamana
nawe kila wakati.
Muhubiri
3:1-8
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na WAKATI
kwa kila kusudi chini ya mbingu. WAKATI wa kuzaliwa, na WAKATI wa kufa; WAKATI
wa kupanda, na WAKATI wa kung'oa yaliyopandwa; WAKATI wa kuua, na WAKATI wa
kupoza; WAKATI wa kubomoa, na WAKATI wa kujenga; WAKATI wa kulia, na WAKATI wa
kucheka; WAKATI wa kuomboleza, na WAKATI wa kucheza; WAKATI wa kutupa mawe, na WAKATI
wa kukusanya mawe; WAKATI wa kukumbatia, na WAKATI wa kutokumbatia; WAKATI wa
kutafuta, na WAKATI wa kupoteza; WAKATI wa kuweka, na WAKATI wa kutupa; WAKATI
wa kurarua, na WAKATI wa kushona; WAKATI wa kunyamaza, na WAKATI wa kunena; WAKATI
wa kupenda, na WAKATI wa kuchukia; WAKATI WA VITA, NA WAKATI WA AMANI.
MSINGI
WA SOMO
1Tim.
4:8 -10
Kwa maana kujizoeza kupata nguvu
za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule
utakaokuwapo baadaye. Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika
kabisa; kwa maana twajitaabisha na kujitahidi KWA KUSUDI HILI, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye
Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.
Wafilipi
2:13
Kwa maana ndiye Mungu atendaye
kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake
jema.
Yeremia
29:11-14
Maana
nayajua MAWAZO NINAYOWAWAZIA ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya
mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.NANYI MTANIITA, mtakwenda na
KUNIOMBA, nami NITAWASIKILIZA. NANYI MTANITAFUTA na KUNIONA, mtakaponitafuta
KWA MOYO wenu wote. NAMI NITAONEKANA KWENU, asema Bwana, NAMI NITAWARUDISHA
watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote,
na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata
mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka.
MAMBO
MATATU

-
1kor. 2:12 Lakini sisi
hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, MAKUSUDI tupate
kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.
-
Zaburi 92:5 Ee Bwana, jinsi
yalivyo makuu matendo yako! Mawazo yako ni mafumbo makubwa.
- Mika 4:12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana,
wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni.
-
Zaburi 139:17-18
Mungu,
fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi livyo kubwa jumla yake! Kama
ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe.

-
Kutoka 33:15 Naye
akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa.
-
Mathayo 12:30 Mtu asiye
pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.
-
KUTOKA 3:7 – 14
Bwana
akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu
wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao;
maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri,
niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa
na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na
Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena
nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa
kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. Musa
akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa
Israeli watoke Misri? Akasema, Bila
shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii;
utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika
mlima huu. Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na
kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu
akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa
Israeli; MIMI NIKO amenituma kwenu.
-
Mdo. 9: 3-16
Hata alipokuwa akisafiri, ikawa
anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.
Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema,
U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini
simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda. ……………… Basi palikuwapo
Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania.
Akasema, Mimi hapa, Bwana. Bwana akamwambia,
Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda
mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; naye amemwona mtu, jina
lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia
habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako
Yerusalemu; hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote
wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule
kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Maana
nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.

-
Mfanyie
Mungu nafasi katika kutimiza kwako hayo ambayo una uhakika ni makusudi ya
Mungu.
-
Ambatana
na madhabahu ya Mungu
-
Mungu
aone nafasi yake katika kufanikiwa kwako.
-
Tunza
Ibada
Ili Mungu
aonekane kwenye jambo lolote ni lazima aione heshima yake kwanza, na apewe
nafasi ya kuweza kuonekana. Mwanadamu peke yake ndiye mwenye nafasi ya kumfanya
Mungu ajidhihirishe katika eneo lolote.
No comments:
Post a Comment