Wednesday, 16 November 2016

JE, UNAISHI KULINGANA NA KUSUDI LA MUNGU JUU YA MAISHA YAKO?

TAFUTA KUTIMIZA KUSUDI LA MUNGU
KATIKA KILA UNALOLIFANYA.

Utangulizi:

Kila jambo litakalokujia wewe kama mtumishi wa Mungu jua kwamba lina muunganiko na kusudi unalolitumikia kwa wakati huo au unaloelekea kulitumikia. Jambo lolote liwe baya au jema, liwe gumu au jepesi, uwe unalijua au haulijui, liwe la kawaida au lisiwe la kawaida.

Nafasi au fursa zote anazofungua au alizofungua Mungu kwako , vita anavyoleta shetani, hali ya mwili wako binafsi-usumbufu, umbo, sura nk; hali ya kiuchumi, familia uliyotoka, maeneo uliyopita na yote uliyofanya katika maisha uliyoishi ni lazima yawe na matokeo ya namna moja au nyingine katika kusudi unalotumikia au utakalotumikia.
🔃🔃
Kila mahali Mungu anapokupeleka ni lazima pawe na kusudi lake, wakati mwingie kusudi lake ni kukuandaa kwaajili ya kusudi jingine. Kila unalofanya likikufanya utimize kusudi la Mungu  rahisi kuona mafanikio makubwa yakiandamana nawe kila wakati.

Muhubiri 3:1-8
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na WAKATI kwa kila kusudi chini ya mbingu. WAKATI wa kuzaliwa, na WAKATI wa kufa; WAKATI wa kupanda, na WAKATI wa kung'oa yaliyopandwa; WAKATI wa kuua, na WAKATI wa kupoza; WAKATI wa kubomoa, na WAKATI wa kujenga; WAKATI wa kulia, na WAKATI wa kucheka; WAKATI wa kuomboleza, na WAKATI wa kucheza; WAKATI wa kutupa mawe, na WAKATI wa kukusanya mawe; WAKATI wa kukumbatia, na WAKATI wa kutokumbatia; WAKATI wa kutafuta, na WAKATI wa kupoteza; WAKATI wa kuweka, na WAKATI wa kutupa; WAKATI wa kurarua, na WAKATI wa kushona; WAKATI wa kunyamaza, na WAKATI wa kunena; WAKATI wa kupenda, na WAKATI wa kuchukia; WAKATI WA VITA, NA WAKATI WA AMANI.

MSINGI WA SOMO
1Tim. 4:8 -10
Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye. Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa; kwa maana twajitaabisha na kujitahidi KWA KUSUDI HILI, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.
Wafilipi 2:13
Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Yeremia 29:11-14
Maana nayajua MAWAZO NINAYOWAWAZIA ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.NANYI MTANIITA, mtakwenda na KUNIOMBA, nami NITAWASIKILIZA. NANYI MTANITAFUTA na KUNIONA, mtakaponitafuta KWA MOYO wenu wote. NAMI NITAONEKANA KWENU, asema Bwana, NAMI NITAWARUDISHA watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka.

MAMBO MATATU
*     Yajue mawazo ya Mungu juu ya kusudi unalolitumikia au unalojiandaa kulitumikia. (Mawazo Mungu anayokuwazia)
-       1kor. 2:12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, MAKUSUDI tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.
-       Zaburi 92:5 Ee Bwana, jinsi yalivyo makuu matendo yako! Mawazo yako ni mafumbo makubwa.
-       Mika 4:12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana, wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni.
-       Zaburi 139:17-18 Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi livyo kubwa jumla yake! Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe.
*     Hakikisha unamuona Mungu kabla hujaondoka kupiga hatua/ wewe binafsi uhakikishwe katika hilo unaloliendea.
-       Kutoka 33:15 Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa.
-       Mathayo 12:30 Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.
-       KUTOKA 3:7 – 14
Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri? Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii; utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu. Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n'nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenituma kwenu.

-       Mdo. 9: 3-16
Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda. ……………… Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania.
Akasema, Mimi hapa, Bwana. Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu; hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.

*     Mwandalie Mungu mazingira ya kuonekana unapoendelea. –“nami nitaonekana kwenu...”
-       Mfanyie Mungu nafasi katika kutimiza kwako hayo ambayo una uhakika ni makusudi ya Mungu.
-       Ambatana na madhabahu ya Mungu
-       Mungu aone nafasi yake katika kufanikiwa kwako.
-       Tunza Ibada

Ili Mungu aonekane kwenye jambo lolote ni lazima aione heshima yake kwanza, na apewe nafasi ya kuweza kuonekana. Mwanadamu peke yake ndiye mwenye nafasi ya kumfanya Mungu ajidhihirishe katika eneo lolote. 

No comments:

Post a Comment

MWANAUME KWENYE NAFASI YA "MUME"

Mume ni mwanaume aliyeoa kwa kuzingatia vigezo na taratibu za kijamii, kishria na za kiroho. Mume si rafiki wa kiume (boyfriend), hawara, wa...

Powered By Blogger